SUBSCRIBE TO OUR YOUTUBE CHANNEL-Shec Media.........LIKE OUR FACEBOOK PAGE-Shec Media..... FOLLOW US ON INSTAGRAM-@shecmedia_tz........WHATSAPP NUMBER +255 752 0133 43

Friday, December 1, 2017

ARUSHA: Madereva Wawatelekeza Abiria na kukimbia: Kisa kukwepa kupimwa Ulevi!


Jeshi la polisi mkoani Arusha kikosi cha usalama barabarani lilikua likiendesha opereshini ya kuwapima madereva wote ulevi ambapo zaidi ya madereva 100 walipimwa huku wengine wakiamua kuyatelekeza magari yao na abiria ili kukwepa kutiwa nguvuni kutokana na ulevi.
Baada ya madereva kutelekeza magari yao, ndipo wamilii wa magari hayo wakaamua kufanya jitihada za kutafuta madereva wengine ili kuwezesha abiria kuendelea na safari zao.
Hali hii ilisababisha abiria wengi kucheleweshewa safari zao na kusababisha malalamiko mengi. Hata hivyo wengi wa abiria wamelipongeza jeshi la polisi na kuwasihi operesheni hiyo iwe endelevu pamoja na kusimamia uzembe wa madereva ili kuepusha ajali za barabarani, hasa msimu huu wa sikukuu za christmas na mwaka mpya.
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha Bw. Joseph Charles amesema kuwa licha ya madereva hao kuwatoloka na kutokomea kusikojulikana, bado wataenelea kuwasaka na kuwachukuliahatua kali za sheria ili kukomesha tabia hii ya ulevi na uzembe kwa madereva.

No comments:

Post a Comment